2015-08-13 15:50:00

Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Wakristo Wafanyakazi


Mkutano wa Wakristo Wafanyakazi walenga katika  kujenga mshikamano na udugu endelevu katika mwa jamii

"Kujenga jamii ya haki, udugu endelevu ni hoja inayotazamwa kwa makini na Mkutano wa Chama cha Wakristo Wafanyakazi, uliofanyika mjini Ouagadougou Burkina Faso hadi Agosti 14 2015. Huu ni Mkutano wa Dunia, wa chama cha Wafanyakazi Wakristo, (MMTC), ambao kwa mwaka huu umefanyika kwa fadhila za  wafanyakazi Wakristo wa Ouagadougou, na kuhudhuriwa na wajumbe wanachama kutoka Burkina Faso yenyewe, pia kutoka Benin, Ivory Coast, Cameroon, Ghana, Madagascar, Mali na Uganda. Mkutano unalenga kutoa azimio lake la mwisho kwa ajili ya ufanyaji upya jamii ya leo.

Kati ya yale yaliyo jadiliwa ni pamoja na kupambana na utofauti unaotokana na wengine kusahaulika katika hatua za maendeleo ya jamii.. Mkutano huu ulifunguliwa kwa Ibada ya Misa iliyoongozwa na Kardinali  Philippe Ouédraogo, Askofu Mkuu wa Oaugadogou, ambaye katika  hotuba yake, alionyesha kuwa ujenzi wa mshikamano na udugu endelevu ni ndoto ya kanisa kwa ajili ya kuleta umoja katika maisha ya kijamii.  Kwa kufanya hivyo, Kardinali alielezea matumaini yake kuwa, chama hiki cha Wakristo Wafanyakazi, kitaweza saidia kupambana kutojali kwa  matajiri ambao wana macho zaidi ya kuona yale yanayowazunguka katika  changamoto kubwa ya umaskini na ufukara.

Wengine waliokwisha toa mchango wao katika mkutano huu ni pamoja Timothée Ody, Rais wa Uratibu wa Mmct Afrika: ambaye akilalamikia uwepo wa dunia iliyojaa dhulma, ubinafsi na choyo. Hasa alisisitiza juu ya mwelekeo wa sasa wa uwepo wa siasa yenye kupoteza hisia ya haki na dhidi ya mfumo wa kiuchumi ulio  kinyume na haki za kijamii.  Kwa hiyo ametoa wito kwa jamii  kuzingatia utendaji wa  usawa na manufaa ya wote. "

Na Charo Castelló Alfaro, ambaye ni Mwenyekiti mwenza wa Mmct,  yeye anasema,  inawezekana kabisa kuleta mabadiliko chanya duniani, iwapo jamii itazingatia kutekeleza sera ya haki hasa katika ugawaji wa mali  na haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Chama hiki cha Wakristo Wafanyakazi cha Dunia , kina wanachama wake  katika nchi 79 za pande mbalimbali za dunia. Wazo la kuanzishwa kwa Chama hiki lilianzishwa kwa mara ya kwnaza na wafanyakazi Wakristo wa  Ujerumani, Austria, Ubelgiji, Ufaransa, Uholanzi na Uswisi kwa lengo la  kudumisha mafunzo, elimu na uinjilishaji, kwa mujibu wa mwongozo wa mafundisho ya kijamii ya Kanisa. Chama kilichoanzishwa rasmi Roma, mwaka 1966, sambamba na kumbukumbu ya  mwaka wa 75 tangu Papa Leo XIII,  alipoweka saini  waraka wa Rerum Novarum,  uliolenga katika harakati za  wafanyakazi, ajira, ukosefu wa ajira, wastaafu na akina mama wa nyumbani.

Papa Leo XIII katika waraka wake huu wa Rerum Novarum, uliopelekwa kwa Wakuu wote wa Kanisa, Maaskofu Maaskofu wakuu , Mapatriaki na wakuu wengine wa kiserikali wenye kuwa na uhusiano naKiti kitakatifu hasa unazungumzia juu ya utendaji wa haki na wajibu katika kazi.
Unalenga kutoa tafakari kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya kiroho, kwa ajili ya kukomesha uwepo wa vurugu na maonevu katika maeneo ya kazi .

 








All the contents on this site are copyrighted ©.