2015-03-03 15:25:50

Tujalie moyo unaofahamu kupenda!


Mama Kanisa anatufundisha kwamba, Moyo ndipo mahali ambapo nipo, ni kiini cha maisha ya mwanadamu yaliyofichika, kisichoweza kufikiwa na akili ya kibinadamu, ni Roho ya Mungu peke yake inayoweza kuupima na kuufahamu moyo. Moyo ni mahali pa uamuzi, penye kina zaidi kuliko maelekeo yetu ya kiroho. Ndipo mahali pa kweli, pale ambapo mwanadamu anachagua uhai au kifo.

Moyo ni mahali pa kukutania, kwa sababu kama sura ya Mungu, mwanadamu anaishi katika mahusiano na maagano. Kumbe, moyo ni mahali patakatifu sana panapotakiwa kulindwa na kutunzwa!

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anawakumbusha kwamba, moyo usiojua kupenda unakuwa mgumu na kunyauka. Baba Mtakatifu anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kumwomba Mwenyezi Mungu awajalie moyo unaofahamu kupenda!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.