2014-12-18 14:57:46

Jifungeni kibwebwe kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa!


Tanzania inapoendelea kusherehekea Miaka 53 tangu ilipojipatia uhuru wake wa bendera kutoka kwa Mwingereza inayo mambo mengi ya kujivunia, hata kama bado kuna changamoto nyingi zinazowakabili watanzania. Bwana Salvatory Mbilinyi, Afisa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Italia katika mahojiano maalum na Radio Vatican anasema kwamba, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mchakato wa kuwaletea watu wake maendeleo endelevu! RealAudioMP3

Kuna mafanikio makubwa katika sekta ya elimu, afya na maendeleo ya watu yaliyokwisha kupatikana nchini Tanzania kupitia katika Serikali za awamu mbali mbali. Kuna haja ya kuendelea kudumisha misingi ya haki, amani na mshikamano wa kitaifa kwa kutambua kwamba, wote ni watanzania na tofauti zao za kidini kisiwe ni kisingizio cha chuki na uhasama. Watanzania wanapaswa kuendelea kujibidisha zaidi katika maboresho ya kiuchumi kwani hii ni changamoto kubwa kwa watanzania wengi kwa nyakati hizi.







All the contents on this site are copyrighted ©.