Balozi wa Tanzania kuwasilisha hati za Utambulisho mjini Vatican
Balozi Filippo Marmo, ni kati ya Mabalozi wapya wasiokuwa wakazi wanaotarajiwa kuwasilisha
hati zao za utambulisho kwa Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 18 Desemba 2014.
Balozi Marmo, hivi karibuni aliteuliwa na Rasi Jakaya Kikwete wa Tanzania kuwa ni
Balozi mpya wa Tanzania nchini Ujerumani na hivyo kadiri ya mapokeo anakuwa pia ni
Balozi wa Tanzania mjini Vatican.
Akizungumza
na Jumuiya ya Wanafunzi Wakatoliki Watanzania wanaosoma mjini Roma, Bwana Salvatory
Mbilinyi, Afisa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Italia amethibitisha kwamba, Balozi
Marmo anatarajiwa kuzungumza na Makleri, Watawa na Waseminari wanaoishi Roma, hapo
Jumamosi, tarehe 20 Desemba 2014. Kwa sasa mipango inaendelea kukamilishwa, ili kufahamu
ni mahali gani ambapo wanaweza kukutana na kuzungumza kwa pamoja, wakati huu Balozi
Marmo anapoanza utume wake kama Balozi wa Tanzania mjini Vatican.