Zaidi ya watu 850 wameathirika kutokana na kulipuka kwa Volkano Cape Verde
Kardinali Theodore Adrien Sarr, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dakar, Senegal anawaalika
waamini na watu wote wenye mapenzi mema kujitokeza ili kuwasaidia wananchi wa Cape
Verde, walioathirika kutokana na mlipuko wa Volkano nchini humo. Anawataka waamini
kutoka kila Parokia kukusanya mchango utakaopelekwa nchini Cape Verde, ili kusaidia
juhudi za kuokoa maisha ya watu wengi ambayo kwa sasa yako hatarini.
Ombi
hili la Kardinali Sarr ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Shirikisho
la Mabaraza ya Maaskofu Afrika Magharibi, katika mkutano wake uliofanyika hivi karibuni
huko Tambacounda, Senegal. Tarehe 23 Novemba 2014, Volkano ililipuka na kusababisha
maafa makubwa kwa watu na mali zao nchini Cape Verde. Zaidi ya watu 850 wamehamishwa
kutoka kwenye makazi yao kwa kuhofia usalama wa maisha na mali zao.