2014-11-27 15:11:59

Ijumaa Papa kuanza ziara ya Kimtaifa ya Sita nchini Uturuki


Papa Francisco Ijumaa hii tarehe 28 Novemba 2014, anaanza ziara Kitume ya Sita kimataifa, ambamo atakuwa Uturuki kwa siku tatu. Siku ya Jumatano, mara baada ya Katekesi yake, Papa alitoa ombi kwa waumini,kwamba anahitaji sala na maombezi yao, ili kwamba, ziara hii anayoifanya katika nafasi ya Petro , kumtembelea ndugu yake Andrea, iweze kuzaa matunda ya amani, mazungumzo ya dhati kati ya dini na mapatano katika taifa la Uturuki.

Ziara hii kitume ya siku tatu, inatajwa kuwa na maana kubwa katika mtazamo wa kiekumeni na mahusiano ya kati ya dini. Ratiba ya ziara hii inaonyesha kwamba, Ijumaa tarehe 28 Novemba , atakuwa Ankara, na kisha 29 na 30 Novemba, atakuwa Istanbul ambako, atakutana Patriaki wa Kiekumeni, wa Constantinople, Bartholomew I, kwa ajili ya kushiriki katika maadhimisho ya Sikukuu ya Mtakatifu Andrea.

Safari ya Uturuki hivyo ni kuendeleza utamaduni ulioanzishwa na watangulizi wake kutembelea Uturuki, na Patriaki wa Constantinople, ziara ya kwanza ilifanywa na Papa a Paulo VI Julai 1967, na kisha Papa John Paul II, Novemba 1979, na Papa Benedict XVI, Novemba 2006.
Msemaji wa Vatican Padre Federico Lombardi , akirejea ziara hii anasema , ni wazi nchi yoyote inayotembelewa na Papa, huwa makini na usalama wa ugeni huu. Na ndivyo ilivyo sasa nchini Uturuki, kumekuwa na majadiliano na mikutano mingi baina ya dini, kwa sababu Uturuki ni nchi yenye kuwa na Waislamu wengi, na kuna jumuiya ndogo Wakatoliki. Na kama ilivyo siku zote wakati wa safari za Papa nchi za Nje, huwa makini. Na katika ziara hii, Papa anakwenda kukutana na Mkuu wa Kanisa la Upatriaki wa Kiekumeni wa Constatinople , Partiaki BartholewI, kama hatua ya maendeleo katika mazungumzo ya kidugu na urafiki wa muda mrefu.
Hivyo ziara hii itakuwa na tabia za kiekumeni ambamo Papa atashiriki katika matumkiio mbalimbali muhimu ya kukutana na watu mbalimbali kama ilivyoandaliwa na wenyeji wake. na akiwa mjini Istanbul, ambamo kati ya mengine ataweka sahihi katika azimio la Pamoja .
Ratiba kwa ujumla inaonyesha kwamba, Ijumaa Papa Francisco baada ya kupokelewa kwa heshima za kitaifa atatembelea jengo la makumbusho la Ataturki na kukutana na Rais a Jamhuri ya Uturuki na viongozi wa kiserikali . Kwa siku ya Jumamosi, Papa ataelekea katika mji wa Ankra, ambako atatembelea Jengo la Makumbusho la Mtakatifu Sofia. Msikiti wa Sultan Ahmet, na atashiriki katika Ibada ya Kiekumeni katika Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu , na baadaye kuwa na sala za kiekumeni katika Kanisa Kuu la Mtakatifu George na kukutana katika hali ya faragha na Patriaki BartholewI
Kwa Jumapili Papa kati ya mengine ataongoza Ibada ya Misa katika hali ya faragha katika jengo la Uwakilishi wa Kitume. Na atakutana na Rabbi Mkuu wa Uturuki , Isak Haleva, nakushiriki katika Ibada katika Kanisa la Mtakatifu George ambalo ni muhimu katika Makainsa ya Kiotodosi.
Papa atarejea Vatican Jumapili jioni.







All the contents on this site are copyrighted ©.