2014-11-26 14:54:06

Kanisa ni mwendelezo wa safari yake kuekelea Ufalme wa Mbinguni - Papa


Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, unatukumbusha sisi sote kwamba, Kanisa halina mwisho lakini huendelea kutembea katika njia ya historia yake ya Ufalme wa Mbinguni, likiwa mbegu na mwanzo wa safari hiyo. Ni maelezo ya Papa Francisko kwa mahujaji na wageni waliokusanyika kusikiliza mafundisho yake Jumatano hii mjini Vatican.

Papa alilenga katika historia ya safari ya wokovu , kwamba, safari hii itakamilika nyakati za mwisho.... wakati ulimwengu utakapo badilika na kumezwa na furaha, amani na upendo wa Mungu katika dunia ya kimbingu ya Yerusalem mpya.

Maelezo ya Papa pia yalilenga katika mwendelezo wa uhusiano uliopo katika utendaji na umoja kati ya kanisa na dunia na kanisa na Mbingu kupitia umoja na wale walio tutangulia kuondoka katika maisha haya ya kimwili. Roho zilizo Mbinguni ambazo hutusaidia sisi kwa maombezi yao, wakati sisi pia tunapoziombea roho zilizoko toharani, kupitia kazi za matendo mema, sala na kushiriki katika Ibada ya Ekaisti.

Kama wana wa Kanisa, basi, tofauti si kati ya wale waliokufa na walio hai , lakini zaidi ni kati ya walio ndani ya imani ya Kanisa ya wale walio nje ya kanisa , watu wasioamini kwa Kristo. Mtakatifu Paulo anatuambia sisi kwamba,si tu ubinadamu utakaowekwa huru dhidi ya maovu lakini viumbe wote. Viumbe wote vitaweka huru katika ukamilifu, ukweli na uzuri wake.

Papa ameutaja kuwa huo ni mpango wa Mungu kwa binadamu, katika kutembea kwenye njia ya maisha, njia yenye msaada kwetu, na ishara ya furaha katika imani na matumaini ya watu wote wanaosadiki kwa Mungu.










All the contents on this site are copyrighted ©.