Rais Napolitano wa Italia, ateta na Papa Francisko kwa faragha!
Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 21 Novemba 2014 majira ya jioni akiwa kwenye
Hosteli ya Mtakatifu Martha iliyoko mjini Vatican alikutana na kuzungumza na Rais
Giorgio Napolitano wa Italia kwa faragha, ziara ambayo haikuwa kwenye ratiba ya shughuli
za kawaida za Baba Mtakatifu kwa siku ya Ijumaa.
Padre Federico Lombardi anasema
kwamba, mazungumzo haya ambayo yamedumu kwa takribani saa moja, yamefanyika katika
hali ya urafiki na maelewano kati ya viongozi hawa wawili.