2014-11-22 14:52:10

Mh. Padre John Yaw Afoakwa, ateuliwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Obuasi, Ghana


Baba Mtakatifu Francisko, amemteua Mheshimiwa Padre John Yaw Afoakwa kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Obuasi, Ghana. Kabla ya uteuzi huu, Askofu mteule alikuwa ni Gombera wa Seminari ya Jimbo la Obuasi, GHana. Alizaliwa tarehe 26 Januari 1955 hukoAkrokerry, Jimbo Katoliki la Obuasi.

Baada ya masomo yake ya awali na sekondari alijiendeleza katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbaniana, kilichoko Roma, kunako mwaka 1983 na baadaye aliendelea na masomo yake ya kidini na kuhitimu kunako mwaka 1986 na kuanza masomo ya kitaalimungu katika Seminari kuu ya Mtakatifu Peter, iliyoko Cape Coast. Akajiendeleza tena kwa masomo ya juu kwenye Chuo Kikuu cha Ghana, kilicho mjini Accra ambako alijipatia shahada ya kwanza katika masomo ya jamii.

Baada ya majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe11 Julai 1992, akiwa ni Padre wa Jimbo la Kumas, Ghana. Jimbo la Obuasi lilipozinduliwa, kunako mwaka 1995Askofu mteule Afoakwa akahamia jimboni humo. Katika maisha yake kama Padre amewahi kuwa: Mwalimu na mhudumu wa wagonjwa; Mkurugenzi wa Idara ya Katekesi Jimboni Obuasi, Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Gombera; Paroko msaidizi na mwalimu wa shule kadhaa Jimboni mwake.

Hadi kuteuliwa kwake na Baba Mtakatifu Francisko kuwa Askofu mpya wa Jimbo Obuasi, Ghana alikuwa ni Gombera wa Seminari ya Mtakatifu Louis, Jimboni Obuasi, Ghana.







All the contents on this site are copyrighted ©.