2014-09-22 12:12:06

Kanisa nchini Uingereza lajibu wito kwa Uinlilishaji mpya


Kanisa la Uingereza kujibu wito wa Papa Francisco
Kanisa la Uingereza limejibu wito wa Papa Francisco alio utoa kwa Jumuiya zote zitafute njia za kufanya kwa ajili uinjilishaji katika nyakati za sasa. Imewezekana kufanikisha ombi la Papa kupitia mpango wa Parokia ya Mtakatifu Maria Mjini Grimsby Uingereza, ambapo waamini wameongezeka idadi ya kwenda katika ibada Misa.
Katika kufanikisha tukio hili vifaa muhimu vya unjilishaji vilisambazwa katika Parokia za Uingereza na Wales, kwa ajili ya maandalizi ya tukio la siku ya umissionari Jumapili 21Septemba ikiwa na kaulimbiu Uinjilishaji, katika moyo wa familia”. Taarifa kutoka katika “gazeti la Oservatore Romano” limemkariri Askofu wa Arundel na Brighton Munsinyo Kieran Thomas Conry, ambaye ndiye mhusika wa kitengo cha uinjilishaji.
Wajumbe wa kamati hiyo ya mpango, Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Maria wa Bahari, Padre Clare Ward na padre Joe Wheat na Ann Casson waliendesha mafunzo muhimu kwa waamini kama njia mpya ya uinjilishaji.
Askofu aliongeza kwamba walikuwa wanafahamu waamini wengi hawaendi katika ibada ya Misa lakini walitaka kujua sababu zake ni nini,baada ya kukutana nao waligundua kuwa hakuna sababu maalumu, bali watu wakiacha kwenda kanisani kwa muda inakuwa vigumu kurudi. Inawaogopesha , na kujisikia aibu ya kuonekana namna gani kanisani, aliongeza Askofu Conry
Katika mpango wao wenye jina “kuvuka kizingiti” waliamua kuwapa matumaini wana parokia ili kuweza kuwafikia waatoliki ambao wako mbali na kanisa ili wapate kurudi , kwani kanisa linalowapokea na linawahtaji. Haijalishi wingi wao wa kurudi kanisani, la muhimu wao watambue kwamba kanisa linawasubiri daima. Aliongeza Askofu.
Naye mkurugenzi aliyetengeneza mpango huo wa iunjilishaji wa Baraza la Maaskofu Uingereza wa parokia tano za Lincolnshire na kanisa kuu la Nottinghan alisema , kile tunachojali ni ule uhusiano wa moja kwa moja na wakristo, wakristo wanaoudhuria kanisa wanapaswa wajisike vizuri, bila kuyumba , katika mioyo yao, ili kuweza kuwakaribia hata wengine walio mbali na kanisa.
Alitoa mfano jinsi walivyofanya kuwavutia warudi kanisania akisema kuwa ,kitu kilichofanyika ni njia ndogo na hasa ile ya matukio yao ya kila siku kwa kupitia utamaduni wa siku ya Mtakatifu Teresa wa mtoto Yesu. Vilevile Kanisa kuu la Nottingham liliamua kufungua milango kila siku jioni kuabudu Ekaristi Takatifu.
Aliendelea kwa njia hizi kumefanya kuongezeka kwa waamini katika parokia kufikia asilimia miamoja. Kwa upande wa kitengo cha unjilishi ni mwafaka na muhimu kujifunza njia zaidi za kumfikia aliyepoteza njia yake ya imani.
Pamoja na mafaniko hayo kwenye mpango huo wa uinjilishaji katika Parokia hizi tano Paund 600 za Uingereza zilitolewa na Baraza la maaskofu katoliki la Uingereza na Galles . Idadi ya waamini wengi walioanza kurudi katika kanisa na hasa kwenye mkesha wa pasaka ni waamini kutoka Parokia ya Mtakatifu Maria juu ya Bahari Grimsby eneo ambalo linahesabika kuwa la nne kwenye umasikini nchini Uingereza.
Vilevile Padre Joe Wheat alisema kwamba kuongezeka kwa watu hao kulitokana na kuwakaribisha wazazi na watoto wao wadogo katika shughuli mbalimbali za kuchora na kutengeneza sanaaa kwa kipindi cha pasaka, ambapo pia walipaka rangi mayai kama utamaduni wa sehemu nyingi za Ulaya.
Aliendelea ya kwamba; walikuwa wakisubiri watu kama ishirini tu lakini , na matokeo yake wakafika watu 80, na kipindi cha sikuku ya kuzaliwa kwa Bwana,waliweza kuweka matangazo wa kuwajulisha juu ya misa itakayofanyika usiku kwenye mwanga wa mshumaa jambo ambalo liliwavutia wengi hadi watu miamoja waliweze kudhuria misa takatifu ya Noel.
Njia ya kuwagawia karatasi mlangoni kabla ya kuanza misa ili wafutile nyinmbo na kujibu sehemu zote za sala zimewezakusaidia waaamini, vilevile maandalizi ya hija na kufanya njia ya msalaba wakzingukia mitaa na miji ni mpango ulio wasaidia waamini kujitokeza na kushiriki , ni ishara ya kuonyesha uwep wa wakristo aliongeza.
Kwa hayo yote Askofu Conry alimazia akikumbusha kwamba Kazi inayofanyika siyo ile ya kutaka kuwaeleta wote kanisani bali kwa nguvu, shughuli hiyo kichungaji ni kwamba waamini wajisikie wanathamaniwa na Kanisa , na Kanisa linawasubiri kushiriki katika maisha yao kila na zawadi msingi za maisha.








All the contents on this site are copyrighted ©.