Baada ya mafuriko Kashmir imeporomoshwa “ground zero”- Askofu
Shirika la habari la Fides limemnukuu Askofu Peter Celestine , akieleza kwamba, "Hali
ya Jammu na Kashmir baada ya maafa mabaya ya mafuriko ambayo hayajawahi kutokea katika
historia ya eneo hilo, maisha ya watu yamerudishwa nyuma katika hatua ya mwanzo “ground
zero”, yakiwa yamepinduliwa kabisa na kuingizwa katika ufukara wa kupindukia. Wakristo
ni kati ya waliokumbwa vibaya na mafuriko hayo.
Askofu Peter Celestine, wa
Jimbo Katoliki la Jammu-Srinagar, ametoa ombi kwa Jumuiya ya kimataifa kutenda kidharura
kwa ajili ya upatikanaji wa misaada ya misaada ya kibinadamu. Amesema, maelfu ya watu
maisha yao yako katika hatari za kuangmia kutokana na ukosefu wa mahitaji msingi ya
kijikimu. Na kwamba, Kanisa Katoliki, linajaribu kila uwezekano wa kujibu hali hii
mbovu, lakini ni wazi limezidiwa nguvu. Wanahitaji msaada wa kidharura wa chakula
na maji ya kunywa, makazi ya muda, dawa kwa watu walioathirika. Karibia asilimia 90
ya walioathirika ni familia za Kikristo. Licha ya watu hao pia mali za taasisi nyingi
za Kanisa zimeharibiwa na hivyo hasara ni kubwa.
Eneo la Malakar Sudan
Kusini limeathirika vibaya na vita-Shahidi aeleza Sista Helen Balatti,
wa eneo la Malakar Sudan Kusini, ametaarifu kwamba, bado kuna hali ya wasiwasi na
ukosefu mkubwa wa utulivu, kwa idadi kubwa ya watu wanaoishi katika mji Mkuu wa Malakar
wa Mkoa wa Upper Nile, ambako kumekuwa kama kituo cha mapigano kati ya Maaskari wa
serikali ya Sudan Kusini na waasi wanaomuunga mkono aliyekuwa Makamu wa Rais, Riek
Machar.
Sista Helena, Mkomboni, ameshuhudia hilo wakati akiwasiliana na shirika
la habari la Fides hivi karibuni, kwamba Mji huo ambao kabla ya machafuko ulikuwa
na wakazi karibia 250,000,kwa sasa umebaki kuwa makao ya wanajeshi. Na kwamba,
pamoja na mikataba ya kusitisha mapigano, hali bado ni teke sana katika eneo hilo.
Hivyo pia hata vyombo vya mawasiliano vimaeathirika, kama ilivyo jionyesha wakati
wa kufungwa kwa Redio Bakhita ya Jimbo Kuu Katoliki la Juba, ambayo imefunguliwa tena
wiki hii, baada ya kufungwa kwa karibia mwenzi mzima. Maelezo ya Sista Helena
yalirejea hasa tukio la mwisho la mapigano ya kivita yaliyotokea karibu na mji wa
Malakar Agosti 21, majira ya asubuhi ambako walisikia sauti ya mabomu, na kama ilivyokuwa
kwa wakazi wengine wa eneo hilo,pia wao Masista waliondoka katika nyumba yao ya kitawa
na kutafuta sehemu nyingine ya kujihifadhi kwa usalama wao. Na kwamba kwa sasa wamepata
uzoefu wa kutosha jinsi ya kukabiliana na ukatili wa wanamgambo wa upinzani. Katika
kipindi cha miezi sita iliyopita, Malakar imeshuhudia mashambulizi kama sita ndani
ya miezi michache
Sista, anaeleza uharibifu unaoendelea katika mji huo wa Malakar
ambao ni mji wa pili kwa ukubwa Sudan Kusini, kwamba, kwa sasa hakuna tena nyumba
za tofali, ila vimebaki vibanda. Cartas Internationalis yakamilisha mkutano
wake. Shirika la Kimataifa la Caritas Internationalis, Alhamisi lilikamilisha
mkutano wake juu ya uratibu wa misaada inayotolewa wakati huu wa mgogoro katika Mashariki
ya Kati. Viongozi Caritas wa Mashariki ya Kati, hasa walilenga juu ya utoaji
wa msaada wa kuonekana kwa wagonjwa mahututi, na wale wanaosumbuliwa na kiwewe cha
ukatili wa vita. Mkutano huu wa siku tatu, ulifanyika mjini tarehe 15-17 Septemba
na wajumbe walijadili hasa uratibu kikanda na kimataifa kukabiliana na mgogoro wa
katika Mashariki ya Kati.
Katibu Mkuu wa Caritas Internationalis, Michel Roy
amesema, walilenga hasa katiak wajibu wao wa kuipa tumaini jamii ya Mashariki ya Kati,
na utoaji wa misaada kwa matawi ya Caritas ya Mashirika ya Kati, katika ngazi
ya kitaifa, kikanda na kimataifa, bila kujali tofauti za kidini , bali katika kuhimiza
utu na haki za baindamu zinaheshimiwa, ili kwamba, kila mtu awe na uhuru wa kuishi
kwa amani na jirani zao. Waziri wa zamani wa serikali Damianos Kattar kutoka Lebanon
alieleza kuwa mahitaji ni makubwa sana, kiasi kwamba peke yao hawaezi kitu. Alifafaanua
kwamba , nchini Syria pekee, leo hii inahitaji kiasi cha dola bilioni $ 100 kukidhi
mahitaji msingi. Na itachukua miaka kati ya 15-25 ujenzi kuijenga tena nchi baada
ya vita hivi. Wakati huohuo, watu wenye msimamo mkali Iraq na Syria wanaendelea kueneza
unyama huu wa kimbali na utakaso wa kidini katika maeneo wanayo yadhibiti.. Na hali
ya Wapalestina ni kama wanaishi katika gareza wazi,wakinyimwa haki ya utu na hadhi
na ardhi yao. Mkutano huu ulihudhuriwa na Askofu Shlemon Warduni, Rais wa Caritas
Iraq, na Padre Raed Abusahliah, Askofu Antoine Audo, Rais wa Caritas na Wawakilishi
kutoka Syria na katika Jordan, Lebanon na Uturuki.
Wakristo katika Nchi Takatifu
wanaishi chini ya uvuli wa Msalaba wa Kristo, alama ya mateso ya hali ya juu Mashariki
ya Kati, alisema Fr Raed Abusahliah, ambaye aliendelea kusema Wakristo wazawa wa eneo
hilo, kuondolewa makwao, itakuwa janga kwa dini zote katika kanda hiyo na dunia
kwa ujumla. Mateso ya watu Wakristo wa Yazidis, inakuwa ni mfano halisi wa mateso
na wasiwasi, unoawapata waamini wa dini zingine ambao ni wachache katika mikoa mingine
kama Palestina na ukanda wa Gaza.
Ebola yaweza kudidimiza uchumi wa
Afrika Magharibi Kuzuka Ebola kunaweza kuathiri uchumi wa nchi za Afrika
Magharibi hasa Guinea, Liberia na Sierra Leone, ambazo zimeshambuliwa vibaya na virusi
vya ebola, Benki ya dunia imesema.
Taarifa ya Benki hiyo inasema , athari
za virusi vya ebola kiuchumi, viko katika mwelekeo wa kuongezeka zaidi katika mataifa
hayo ambayo tayari yako katika myumbo tete wa kiuchumi, ambako mpaka sasa virus vya
ebola vimekwisha ua watu 2461 Afrika Magharibi.
Rais wa Marekani Barack Obama
hivi karibuni alikuita kuzuka vya virus vya ebola kuwa "tishio kwa usalama wa kimataifa,"
na alitangaza Marekani ina wajibu m kubwa katika kupambana na virusi vya ebola kama
ilivyokuwa kupambana na ukimwi. Hatua zinazo chukuliwa na Marekani, pamoja na kupeleka
askari wake katika mikoa iliyoatharika kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vituo vya afya
zaidi vitakavyoshughulika na huduma mpya ya afya.
Alhamis hii Baraza la Usalama
la Umoja wa Mataifa, lilikuwa na kikao cha dharura kujadili janga hili. Ilitazamiwa
mkutano kukamilika na azimio linalo dai jumuiya ya kimataifa iingilie kwa nguvu zaidi,
tatizo hili, na kuzitaka nchi wanachama kupeleka msaada wa madaktari na kufungua vituo
zaidi vya kukabiliana na virusi. Pia azimio linatazamiwa kuzitaka nchi kuondoa vikwazo
vya kusafiri kutoka na kuingia yenye kwua na wagonjwa wa ebola, kwa maelezo ya Viongozi
wa Umoja wa Mataifa kwamba , hakuna sababu za kufanya hivyo kwa nyakati hizi. Uchambuzi
wa Benki Kuu unaonyesha kwamba, uchumi wa nchi zilizoathirika na virus vya ebola utadodoka
kwa mabilioni ya dola ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao wa fedha. Na kamba mpaka sasa
tabiri zinaonyesha kwamba, uchumi utapungu a kwa asilimia 2.3 Guinea na Sierra Leone
utashuka kwa aslimilia 8.9. Jengo la Joshua wengi wa waliofariki ni Wasauthi Kwa mujibu wa takwimu za Jumatano , wengi wa waliofariki katika jengo la Joshua
lililo poromoka Ijumaa iliyopita, ni kutoka Afrika Kusini. Inatajwa kati ya maiti
zilizopatikana kuna miili 67 ya Wasauthi. Jengo lililokuwa likitumika kama Hosteli,
ni mali ya mhubiri Maarufu wa Nigeria , Mwinjilisti Joshua, la nje kidogo ya mji wa
Lagos, liliporomoka wiki iliyopita. Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameiita ajali
hii kuwa mbaya katika historia ya maafa kwa Wasauthi hivi karibuni Viongozi wa Nigeria,
wanatajwa kuwa wazito kutoa habari za kuaminika juu ya waliofariki katika ajali hii. Na
katika ujumbe wa rambirambi iliyotolewa na Maaskofu Katoliki wa Afrika Kusini , Mkurugenzi
wa Kitengo cha Mawasiliano katika Baraza la Maaskofu, Br S'milo Mngadi, amesema, Maaskofu
wameonyesha kusikitishwa na ajali hii. Na wanaziombea roho za marehemu zipate kupumzika
mahali pa amani kwa Mungu, familia zao ziweze kufarijika katika ufufuko wa Bwana,
na majeruhi wapate kurejea afya njema.
Pamoja na waliofariki watu wengine
zaidi ya 130 wamebaki majeruhi.tu wengine ni alisema kuwa kujeruhiwa. Hosteli alikuwa
mwenyeji wa Afrika Kusini. TB Joshua ni mkubwa sana maarufu tele-mhubiri katika Afrika.