Caritas yafanya mpango wa dharura kwa ajili ya mafuriko India
Shirika la caritasi hivi karibuni lilitoa habari kuhusu kuomba msaada kwaajili ya
watu zaidi ya milion 3,5 nchini India baada ya mafuriko mabaya yalioyoikumba baadhi
maeneo mbalimbali ya nchi.
Wasiwasi mkubwa ni juu ya watu walio rundikana bila
kuwa nyumba na msaada kwani maeneo mengi ya ardhi na nyumba vilipelekwa na mafuriko
hayo, itachukua muda kuweza kurudia hali na kukarabati maeneo hayo.
Shirika
hili linatoa ripoti kwamba pamoja na juhudi hizo za kuweza kuwasaifda watu walikumbwa
na mafuriko hayo , linahitaji kukusanya kiasi cha euro 768 elfu kwaajili ya kuwasidia
milioni ya watu ambao wamepoteza nyumba na kila kitu, katika maji.
Linaongeza
mpango huko wa dharura unakadiriwa kufanyika ndani ya miezi 8 ukiwa na mategemeo ya
kuwasidia watu 47,000 wa maeneo mabambali ya nchi na hasa waliokumbwa na mafuriko
hayo.
Mpango huo unategemea kujenha na kukarabati nyumba, kuweka nyumba za
dharura kwaajili ya familia zisizo na mahali pa kukaa kwa muda mfupi, na kuboresha
meeneo hasa kwaajili ya afya kwa ujumla.
Na zaidi ya hayo Caritas ina mpango
wa kutafuta miundo mbinu ya teknolojia na kilimo, ikitaka kutoa hata vifaa , mbegu,
na wanyama kwaajili ya maendeleo endelevu katika uchumi.
Hata hivyo pia inahitaji
kuweka mpango wa kuweka akiba kwaajili ya dharuara ya mafuriko iwapo yanaweza kutokea
tena.
Baraza la Maaskofu India laonba Msaada Mwenyekiti wa
Baraza la maaskofu India (CBCI) Kardinali Baselios Cleemis, ameomba watu wote zaidi
ya wakatoliki million 16 India kuwa na ukarimu wa kujitoa kusaidia watu wa maeneo
ya Jammu na Kashimir , maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko.
Katika wakaraka
wake alielelezea wasiwasi mkubwa alio nao kuhusu watu ambao wamepoteza maisha yao,
na wengine wengi kupoteza ardhi, nyumba zao kubomolewa na maji.
Inasemekana
kwamba zaidi ya watu 200 walikufa , na ekari za ardi kupelekwa na mafuriko. Barabara
kuu ya mji zilifungwa kwa siku 9 kutokana barabara nyingi kubomoka au kupelekwa na
maji, kiasi cha hata waziri Omar Abdallah, kuomba msaada wa dharura wa kuomba mashine
za kupamp maji katika maeneo mengi ya makazi ya watu.
Timu za madaktari na
wataalamu mbalimbali wakiwemo wataalumu wa magonjwa ya mlipuko , walipelekwa huko,
na pia Tani 1000 za madawa zinahitajika kumpambana na magojwa ya tumbo kuhala na
pia chakula.Bado katika maeneo ya Ramban na Banihal maelfu ya tani za maji zinahitajika
kukidhi haja ya watu.
Zaidi ya mahema 80 yametayarishwa kwaajili ya watu wasiokuwana
makao, pia juhudi za vikosi vya kuokoa vinaendelea na mpango wa kupeleka mahema mengine
, vyakula , vifaa vya kujifunika nk , lakini pamoja na juhudi hizo watu ni wengi na
vifaa hivyo haviwatoshi alisema Kardianali Baselios.Bado pia tatizo kubwa la njia
za kimawasiliano na hivyo kuhitajika nguvu zaidi ya utengezaji wa barabara hili watu
waweze kufikiwa msaada.
Aliongeza suala la ukosefu wa mahali pa kuishi ni kubwa
kwa watu walio salia na mafuriko kwani zaidi ya nyumba 20,000 zilianguka na nyingine
nyingi zinzahitaji kukarabatiwa.
SIku ya Kimataifa ya Ushirikiano wa
Kisni mwa Sayari ya Dunia Ijumaa 12Sept2014 ilikuwa ni siku ya Kimataifa
ya Ushirikiano wa Kusini mwa Sayari ya Dunia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa , Ban
Ki Moon alisema kuwa siku hiyo ya mwako huu inakuja wakati jamii ya kimataifa ikiwa
kwenye kipindi cha mpito kuelekea ajenda ya maendeleo baada ya mwaka 2015, ambayo
inazingatia ufanisi wa pamoja na uendelevu wa mazingira.
Bwana Ban aliongeza,
pamoja na kupiga hatua kubwa katika kufikia malengo ya maendeleo ya Milenia, (MDGs)
hatua za maendeleo kwenye nchi za kusini mwa dunia bado haziwekwa sawa.Kwasababu
umaskini uliokithiri, ueneaji wa kutokuwepo usawa, utapiamlo na kuwa hatarini kuathiriwa
na majanga ya tabianchi na hewa bado vimeshamiri.
Kwa mujibu wa takwimu za
mseto za Umoja wa Mataifa kuhusu umaskini, watu bilioni 2.2 bado wanaishi katika umaskini
uliokithiri. Aliongeza kuwa watu wapatao bilioni 1.4 –wengi wakiwa kusini mwa sayari
dunia- hawana umeme, huku watu milioni 900 wakiwa hawana maji safi na bilioni 2.6
hawana huduma tosha za usafi kwa ujumla.
Ban Ki moon alisema kuwa ushirikiano
wa Kusini mwa Dunia unatoa fursa nyeti ya kuleta usawa katika ukuaji maendeleo katika
ushirikiano wa kimataifa kuhusu maendeleo endelevu.
Mahitaji ya madini
ya urani itumikayo katika vituo vya nishati kupanda: (IAEA) Mahitaji
ya madini ya urani, malighafi inayotumiwa kama nishati ya vituo vya nguvu za nyuklia
duniani kote, itaendelea kupanda katika siku za karibuni, licha ya kushuka kwa bei
za soko tangu ajali ya kituo cha umeme cha nyuklia cha Fukushima Daiichi nchini Japan
Machi 2011, sambamba na mahitaji ya chini ya umeme kwa sababu ya mtikisiko wa uchumi
duniani.
Haya ni miongoni mwa matokeo ya msingi ya riporti mahususi iliyotolewa
10Sept2014 na Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki pamoja na Kitengo cha nishati
ya Nyuklia cha Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo, (OECD)Ripoti hiyo
ijulikanyo kama Red Book, imeelezea kuongezeka kwa urani, utafutaji na pia uzalishaji
.
Tangu kuchapishwa kwa ripoti ya mwaka wa 2012, asilimia saba ya raslimalia
ya urani imetambuliwa na hivyo kuongeza karibu miaka 10 ya rasilimali zilopo. Inasemakana
kwamba uzalishaji wa urani duniani kati ya mwaka 2010 na 2012 , umeongezeka japo ni
kwa kisai kidogo kuliko kipindi cha miaka miwili ya awali.
Ubia mpya
wazinduliwa kuokoa misitu ya dunia (UNEP,IUCN) Hivi karibuni mwezi huu
Sept2014 ulizinduliwa ubia mpya wa kuokoa misitu ya dunia katika ya Shirika la Mpango
wa Mazingira (UNEP) na Muungano wa Kimataifa wa Kuhifadhi Maliasili (IUCN).
Juhudi
za kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kuboresha maisha kwa kulinda misitu zimepewa
msukumo mpya ambapo uzinduzi huu mefanyika wiki chache Kabla ya mkutano wa kilele
wa hali ya hewa iliyoandaliwa na Katibu Mkuu Ban Ki-moon katika Makao Makuu ya Umoja
wa Mataifa mjini New York ambayo itafanyika tarehe 23 Septemba.
Ushirikiano
huo unalenga kurejesha misitu iliyoharibiwa kwa kuhakikisha kuna tena ekari milioni
150 za misitu ifikapo mwaka 2020. Ushirikiano huo utaleta pamoja mikakati miwili muhimu
ya kimataifa inayoendelea ya kuokoa ardhi iliyomomonyoka, ambayo ni Mpango wa pamoja
wa Umoja wa Mataifa wa Kupunguza Uchafuzi utokanao na Uharibifu wa Misitu, UN-REDD
na Ubia wa Kimataifa kuhusu Kuokoa kwa Ardhi ya Misitu pamoja na kusaidia ufumbuzi
wa nishati safi.
Serikali ya Ujerumani hivi ilitoa dola bilioni 1 za kimarekani
kwaajili mfuko wa mpango wa kupamabana na mabadiliko ya tabianchi ikiwa ni mchang
wa kwanza katika mfuko huo, na michango mingine inategemewa mwezi novemba mwaka huu
wakati wachangiaji watatangaza michango yao kwaajili ya kuimarisha mfuko huo.