2014-09-01 11:10:22

Wakristo: dumuni katika kuwa ladha ya chumvi ya dunia- Papa


(Vatican Radio) Baba Mtakatifu Francisco, siku ya Jumapili alitoa wito kwa waumini na watu wote wenye mapenzi mema kudumu katika kuwa ladha ya chumvi ya dunia, katika huduma mbalimbali, ikiwemo utetezi na utunzaji wa viumbe. Papa alitoa wito huo, akiangalisha katika adhimisho la Siku ya Maaskofu wa Italia, kwa ajili ya Ulinzi na utetezi wa viumbe, ambayo Maaskofu wamechagua mwaka huu, kuzingatia kuelimisha katika huduma kwa ajili ya viumbe. Ni matumaini ya Papa Francisko kwamba kila mtu, kila taasisi, vyama na wananchi - wataimarisha juhudi zao, ili kulinda maisha na afya ya watu na Kuheshimu mazingira na asili.

Papa Francisko alitoa wito huo, baada ya hotuba yake iliyofuatiwa na sala ya Malaika wa Bwana, aliyosali pamoja na mahujaji na mahujaji na watalii waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa kanisa Kuu ya la Mtakatifu Petro Vatican.

Kabla ya sala Malaika wa Bwana, Papa alihutubia juu ya somo la Injili , wakati Yesu alipowaeleza wanafunzi wake juu ya mateso yake, kifo na ufufuo (Mt. 16: 21-27). Papa aliutaja wakati huo kwamba ulikuwa ni wakati muhimu wenye kuonyesha tofauti dhahiri kati ya njia ya Yesu ya kufikiri na ile ya wanafunzi wake , na hasa katika tabia ya Petro. Petro, kiongozi wa mitume kumi na wawili kwa fikira zake za kibinadamu, anamfokea Bwana wake, kwamba hayo hayawezi kumtokea. Papa Francis aliendelea kufafanua, Yesu, kwa upande wake, pia anamkemea Petro , kwa sababu hakufikiri kwa mujibu wa Kazi ya Mungu, ila kwa fikira za utendaji wa kibinadamu, na bila ya kutambua kama ni majaribu na kishawishi cha shetani.

Baba Mtakatifu alisema, Mtakatifu Paulo kwa somo hili, anatuambia sisi katika barua yake kwa Wakristo wa Roma, tusitende kwa mitindo ya ulimwengu huu, lakini kwa kufanya upya akili zetu ili tupate kuushinda mtihani wa maisha kwa kutenda yaliyo mema ya kumpendeza Bwana , na kwa mapenzi kamili ya Mungu (Rum 12:. 2).

"Kwa kweli, aliendelea Papa Francisko, sisi Wakristo tunaishi katika ulimwengu huu tukiwa tumechanganyikana kijamii na kiutamaduni kadri ya hali halisi za wakati wetu, hiyo ni sawa, lakini hii Papa alionya, linaleta hatari ya kutaka kutenda 'kidunia'. Tutapoteza ladha ya 'chumvi ya Ukristo tusipokuwa waangalifu '(cf. Mt 5:13). Papa aliwataka Wakristo kuwa macho na maamuzi yanayotolewa kwa fikira za kunufaisha kidunia tu, mawazo yasiyo mtanguliza Mungu. Alisisitiza kwamba, Wakristo wanapaswa kuwa kinyume na fikira zote potofu, kama Injili inavyofundisha. Na kwamba , nguvu ya Injili bado ni hai ndani ya Wakristo, na ina uwezo wa kubadilisha vigezo vya hukumu za wanadamu, kutathimini maadili, faida zake, na mwelekeo wa mawazo, vyanzo vya msukumo wake na mifano ya maisha yaliyo tofauti na Neno la Mungu na mpango wa wokovu.

Mwisho, Papa kwa upendo Mkuu aliwasalimia wote waliokuwa wakimsikiliza, aliwataja washiriki wa mkutano wa kimataifa wa 5 wa Watunga sheria Katoliki , mkutano uliofunguliwa huko wiki iliyopita Frascati, nje Roma. Aliwahimiza, waishi kwa moyo mkuu jukumu lao nyeti la kuwa watetezi wa watu, kulingana na maadili Injili.








All the contents on this site are copyrighted ©.