Semina ya kimataifa juu ya Michezo kwa ajili ya binadamu
Tarehe 1Sept 2014 katika uwanja wa michezo Olympio wa Roma kutafanyika kandanda ya
michezo kati ya muungano wa madhehebu mbalimbali ya dunia.
Kutokana na fursa
hiyo ya michezo itakayo fanyika Baraza la ushauri na utamaduni la kipapa kwa ushirikiano
, na Ofisi ya taifa ya kichungaji ya muda uria , Ofisi ya michezo na utalii ya Baraza
la Maaskofu Italia, Shirika Yohane Paulo wa Pili kwaajili ya michezo, watakutana
na wahusika wa Taasisi za Kimataifa katoliki za michezo kuwa na siku ya majadiliano,
na kaulimbiu “mchezo ni kwaajili ya binadamu”, <> Ni semina ya siku tatu itakayo fanyika katika
Ofisi ya Baraza la mashauri na utamaduni la kipapa mjini Vatican, na watakao udhuria
ni pamoja na wawakilishi kutoka vyama vya michezo vya kikatoliki vya Marekani, Uingereza,
Italia, Mexico, Slovakia, na Malta
Pamoja na mengi yatakayogusiwa katika mkutano
huo ni pamoja na kuandaa mkutano mkuu wa dunia utakao kuwa na kaulimbiu juu ya
“ Vatican Mkutano wa kimataifa wa Michezo na Imani Septemba 2015 (Vatican Global
Conference on Sport and Faith) Sept 2015. Mkutano huo utakuwa wa kihistoria kufanyika
kwa mara ya kwanza Makao Makuu ya kharifa wa mtume Petro hapa mjini Roma kati ya
viongozi wakuu wa Kimataifa , viongozi wote wa michezo, duniani na viongozi wa dini
kwaajili ya kujadili changamoto zinazokabili michezo duniani. Ndugu wapendwa wasikilizaji
wa Radio vatican , pamoja na kauli mbiu ya semina hii ya “ Mchezo ni kwaajili ya binadamu”
kuanzia matokeo ya utamaduni kufikia kukutana na tamaduni, utakaofanyika 1Septemba
2014; Je tunaweza kukumbuka kitu gani kuhusu michezo katika jamii zetu na katika
tamaduni zetu? Je leo hii michezo ni kwaajili ya binadamu kweli au inavuka mipaka
ya ubinadamu? Ni makala yetu leo ninayotaka tupate kujadiliana kwa pamoja. Kwanza
kabisa katika ujumbe wa video kwenye ufunguzi wa kugombea kombe la dunia la mwaka
huu 2014 huko nchini Brazil Papa Francis alisema mambo muhimu juu ya michezo pamoja
na hayo alitoa kauli kuwa michezo “ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha
ubinadamu na katika ujengani wa jamii ya amani na ya kindugu” Kwa kauli hiyo
yatari tunapata wazo kuu juu ya michezo kwa ujumla ya kwamba michezo imekuwa na lengo
kuu msingi tangu zamani za kale la kujenga undugu na amani.
Kama mchezo ni
chombo cha kuwasilisha tunu ya binadamu mwenyewe, kujieleza mwenyewe, kukubalika mwenyewe
na kujikubali, inamaana kwamba nchi yoyote haiwezakani kutambulikana na utaifa wake
bila kuwa na utamaduni wao, na mojawapo ya viungo vya tamaduni hiyo vinavyounganisha
katika duniani hii ni “michezo”. Mfano kuna baadhi ya mataifa mbali ambayo wameweza
kujitambulisha kwa mavazi, na ishala mbalimbali … ukiona “vazi “ fulani tayari unajua
ni kutoka nchi gani…au ishala fulani kama vile sisi afrika mashariki “wamasai”, tayari
unajua wanatokea wapi, hivyo basi michezo ni chommbo muhimu sana katika kuendeleza
jamiii. Aidha michezo uweza kuwa kielelezo kikubwa na utambulisho wa taifa katika
kutoa burudani, kujenga nidhamu , kujitangaza kiuwezo na kukomaza afya, ya mwili
na akili . Mara ngapi nchi moja na nyingine inajitangaza vipaji vya wachezaji wake
inaposhiriki michezo ya kitaifa na kimataifa (mifanotunayo mingi, sasa hivi tunasikia
ni jinsi gani wachezaji wa mipira watahama kutoka timu moja hadi nyingine mara baada
ya kombe la dunia , maana sasa hivi wako katika soko...)
Kutokana na umuhimu
wa michezo katika jamii kila kipindi cha kihistoria, binadamu amekuwa akishiriki
michezo katika tamaduni mila na sanaa,tunajua michezo ya mila na desturi tangu zamani
, imekuwepo, mieleka, kuruka, kukimbia kulenga shaba ya mishale , kuogelea nk. Ni
michezo iliyokuwa inalenga kujiamini na kuwa na utambulisho wa kila jamii ambayo iliitwa
ya jadi, hata ndugu zetu waliopelekwa kwenye utumwa na kukutana na watu wa mataifa
mbalimbali walieneza jadi zao katika michezo hiyo, iliyowasaidia sana kukabiliana
na matatizo yaliyokuwa yanawakumba katika utumwa huo. Lakini ndugu wasikilizaji
wapendwa baada ya michezo ya kisasa kuingia kama mipira ya miguu, mipira ya meza,
ndondi, mbio, baiskeli,magari ya mashindano, mashindano ya farasi na michezo mingine
mingi historia ya jadi ikalegeza thamani yake, na kuanza kutawaliwa kwanza fedha na
ushindani Hatuwezi kusahau kwamba michezo ya jadi kwanza ilikuwa inalenga undugu
zaidi , urafiki zaidi burudani zaidi ,katika kushirikiana kwa pamoja na kuishi kwa
amani. Leo hii katika viwanja mbalimbali vya mipira, kuna uwoga wa kurudi salama
au kutokurudi salama, ni hatari kubwa. Millenia ya leo inazo changamoto nyingi
ambazo zimejitokeza kwenye michezo kama vile, kinachotangulia ni fedha, na ushindani,
au kuwepo na madharau ya rangi za watu, kutaka kushinda kwa kila njia, wakati mwingine
hata watu wanaofanya michezo hiyo kupenda kutumia hata madawa ya kujiharibu mwili
hili wawe na guvu za kushinda.
Ndugu wasikilizaji wa radio vatican, changamoto
ni nyingi kwani mabadiliko ya jamii yetu wazazi wengi kutowafundisha watoto umuhimu
wa michezo ni nini, kwasabau watoto walio wengi ukisema mchezo kitu cha kwanza kichwani
ni kufikiria kushinda kabla ya burudani na furaha ya kushiriki na wengine, na ndiyo
maana utakuta watoto wengine hawapendi kushiriki michezo kama ngoma muziki akisema
mimi siwezi maana mwenzangu ndiyo aliye na uwezo.
watoto walio wengi wanapokwenda
kwenye michezo tayari wana wazo lazima washinde tu, na kumbe uwajibikaji wa jamii
zetu kuanzia katika familia muhimu sana kuwafundisha tangu utoto umuhimu wa miichezo
ya pamoja kwanza ni kufurahi , kunyosha viuongo kwa ajili ya kutunza afya bora na
siyo tu kushinda na kupokea zawadi. Maana katika mchezo lazima mmoja tu ashinde,
mfano wa hivi karibuni tumeona machozi , masikitiko na majonzi kwenye kombe la dunia.
Katika barua ya kwanza Mtakatifu Paulo kwa wakorinto alijua wazi ushindani
huo wa michezo ambao unaweza kutufanya tusahau misingi na thamani kubwa ya binadamu,
yaani mimi na mwenzangu na Mungu.
Alisema“ Je hamjuhi ya kuwa wale washindanao
kwa kupiga mbio , hupiga mbio wote , lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna
hiyo ili mpate. Na kila ashindaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao ufanya
hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo: bali sisi tupokee taji isiyoharibika” (1Wakor
9,24-26)
Na kumbe michezo ina utajiri mkubwa kwa binadamu si katika bihashara
au malumbano, bali utajiri wa kuunganisha watu, kabila , jamii, taifa na mataifa
nikitoa mfano wa changamoto za zinazokabili nchi za Ulaya ,ukimbizi na uhamiaji kupitia
njia ya baharini , siku hizi tumeona watu wengi na hasa vijana waliopokelewa katika
vituo mbalimbali hapa nchini Italia hata kama hawajuhi lugha ya mahalia , lakini
kinachowaunganisha , ni zile talanta zao walizo nazo za kucheza michezo mbalimbali,
na ndiyo maana ya semina ambayo itafanyika kwaajili ya kuandaa mkutano mkuu wa mwaka
kesho 2015 Michezo izidi kuoboreshwa katika tamaduni zetu, hili iweze kutuunganisha,badala
ya kututenganishe, iboreshe utu kwanza kuliko kujali mali , ndipo tutajenga jamii
ya utu kweli na yenye kupendana kama ndugu.