Mawaziri wa Afya Afrrika Magharibi wajadili mikakati ya kupambana na ebola
Kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola, safari za ndege kuelekea Afrika Magharibi
zilikuwa zimepigwa marufu.Mawaziri wa Afya kutoka nchi za Afrika Magharibi, wamekubaliana
kuondoa upigaji marufu huo wa safari za ndege, na ufungaji wa mipaka kwa nchi zilizoathirika
kutokana na ugonjwa wa Ebola. Mawaziri hao ambao wamekutana mjini Accra, Ghana
kupitia na kuangalia kwa upya mikakati iliyokuwa ikitumika kupambana na virusi vya
ebola na pia wametoa ombi maalum kwa mashirika ya ndege kurejesha safari zao katika
nchi zilizoathirika.
Mawaziri wa afya wamesisitiza mkakati wa pamoja kuwa bado
ni mpango bora kabisa katika kupambana na ugonjwa wa ebola. Mawaziri hao wamezitaka
nchi kutofunga mipaka yao kwa nchi zilizoathirika lakini wabakie kuwa waangalifu.
Pia
wamekubaliana kuongeza raslimali kwa watu ikiwa ni pamoja na kutakiwa wafanyakazi
wa afya kwa haraka , vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo, na vituo vya kuwahifadhi
wagonjwa.
Shirika la Afya la Afrika Magharibi lina wiki moja ya kuandaa hatua
za kuchukua na kuandaa bajeti ili kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa kwa kushirikiana
na Shirika la Afya Duniani na wadau wengine.
Waliodhuria mkutano huo ni Mawaziri
wote wa afya wa kutoka nchi zilizoathirika kutokana na ugonjwa wa ebola za Guinea,
Sierra Leone, Liberia na Nigeria, wengine waliobaki hawakuweza kuhudhuria kutokana
na matatizo ya ndani na matatizo ya usafiri wa ndege ambao umesitishwa katika nchi
zilizoathirika. Mawaziri wa afya wametoa ombi maalum kwa mashirika ya ndege kurejesha
safari za ndege na kuendelea kuruka kwenda katika nchi zilizoathirika. Hata hivyo
wamesisitiza upimaji wa joto la mwili na kuhakikisha usafi wa mikono katika vituo
vya kuingia na kutoka.
SHIRIKA LA AFYA DUNIANI WHO Pamoja na harakati
hizo zinazofanyika, bado kuna ofu ya kuambukizwa watu 20,000 na Ebola, kama shirika
la afya WHO duniani linavyoripoti huko Afrika Magharibi. Shirika hilo la Afya limeonya
kuwa mlipuko huo huenda ukasambaa na kambukiza zaidi kabla haujadhibitiwa.
Kwa
sasa idadi ya waliothibitishwa na kuorodheshwa kuambukizwa ni elfu 3 ingawaje inashukiwa
kuna watu wengi ambao hawajajulikana. Hadi sasa zaidi ya watu 1500 wamefariki
kutokana na mlipuko wa sasa wa Ebola wengi wao wakiwa ni wa kutoka nchi za Liberia,Sierra
Leone na Guinea. Mkurugenzi wa (WHO) katika kanda hiyo - Dr Lious Sambo - ameeelezea
jinsi wafanyakazi katika kliniki za wagonjwa wanavyoanagaika sana wakijaribu kukabilianana
na janga hilo la Ebola. Wauguzi ni wachache na kwa wakati huo wanapaswa kusaidia
haraka inavyowezekana.
TUZIJUE NJIA TANO ZA KUJIEPUSHA VIRUSI VYA EBOLA NA
DALILI ZAKE.
Ebola ni mojawapo ya virusi hatari zaidi ulimwenguni lakini haiambukizwi
kupitia hewa, hivyo basi huwezi kuambukizwa Ebola kama homa ya kawaida. TUZIJUE
NJIA TANO ZA KUJIEPUSHA VIRUSI VYA EBOLA NA DALILI ZAKE.
Ebola ni mojawapo
ya virusi hatari zaidi ulimwenguni lakini haiambukizwi kupitia hewa, hivyo basi huwezi
kuambukizwa Ebola kama homa ya kawaida. Madaktari wanasema kuepuka Ebola ni rahisi
sana iwapo mtu atafuata tahadhari hizi muhimu zaidi: Njia ya kwanza ni sabuni na maji.
Nawa mikono kila baada ya shughuli yeyote kwa kutumia sabuni na maji safi- na utumie
taulo kujikausha. Hili huwa jambo gumu kwa wanaoishi kwenye makazi duni, na walio
vijijini ambako aghalabu maji safi hayapatikani moja kwa moja- lakini ni mbinu iliyothibitishwa
ya kuua virusi vya Ebola.Unachohitaji tu ni sabuni ya kawaida.
Kusalimiana
kwa mikono kunafaa kuepukwa kwa ujumla, daktari Unnis Krishnan wa Plan International
aliarifu BBC, kwamba Ebola husambazwa haraka watu wanapowasiliana ana kwa ana na
maji maji ya kimwili ya waliougua.Na dalili ya ugonjwa huu huchukuwa muda kabla ya
kudhihirika, hivyo inabidi kutumia njia zingine za kujuliana hali.
Njia ya
pili ni hakuna kugusana:Iwapo unashuku kuwa mtu ana Ebola, usimguse. Inaokena
kuwa si maadili mema unapoona unaowapenda wakihisi uchungu na unataka kuwakumbatia
na kuwahudumia, lakini maji maji ya kimwili- mkojo na kinyesi, matapishi, kamasi,
mate, machozi, na mbegu za kiume na majimaji ya uke- vyote huweza kueneza Ebola.
Dalili
za mtu aliyeugua ni joto mwilini, maumivu kwa misuli na viungo, vidonda kooni, kuumwa
na kichwa, na uchovu- kufuatiwa na kichefuchefu, kutapika, na kuharisha, ambapo mtu
huweza kutoa damu pia. Watie watu hao moyo kutembelea kituo cha afya haraka iwezekanavyo.
Pia
ni uamuzi mzuri usiguse nguo au vifaa anavyolalia hao waliougua Ebola- kwani na
Medecins Sans Frontieres anashauri kuwa malazi ya waliougua yanafaa kuteketezwa.
Njia
ya tatu ni kuepuka miili ya wafu: Iwapo unadhani mtu amefariki baada ya kuugua
Ebola, usiguse mwili wao, hata kama ni mila au desturi ya maziko. Baada ya mtu kufa,
bado unaweza kuambukizwa Ebola kutoka kwa miili yao kwani bado inatoa maji maji ya
mwili ambayo huweza kuwa hatari zaidi hata kuliko ya mtu alieugua. Fanya mipango kupata
timu ya walioandaliwa kushughulikia mwili huo haraka iwezekanavyo kwani ni hatari
kuwacha mwili wa mfu kwa muda mrefu katika eneo la makazi.
Njia ya 4. Usile
nyama ya porini Epuka kuwinda, kugusa, au kula nyama ya porini, kwa mfano popo,
nyani na sokwe, kwani wanasayansi wanaamini kuwa hiyo ndiyo chanzo cha maambukizi
kwa binadamu. Hata kama mnyama fulani wa porini huliwa katika eneo lenu na nyama yake
ni tamu epuka myama huyo kwani nyama yake au damu yake huweza kuwa na virusi hivyo.
Na hakikisha vyakula vyote vinapikwa inavyostahili.
Njia ya 5. Usiwe na hofu Kueneza
uvumi huongeza hofu. Usiogope wafanyakazi wa huduma za afya- wako hapo kukusaidia
na kliniki ndipo mahali mwafaka kwa mtu kuponywa- wataongezewa maji na kutulizwa maumivu. Takriban
nusu ya watu walioambukizwa Ebola kufuatia mzuko wa hivi punde wa Ebola walifariki.
Kumekuwepo
na matukio ya madaktari kushambuliwa na watu kutorokwa wanaposhukiwa kuwa na Ebola-
hata wakati wanaugua ugonjwa tofauti. Kuamini matibabu ya kiasili ambayo hayajathibitishwa
kutoa afueni, pia kumechangia ongezeko la kuenea kwa virusi vya Ebola.
"Kinga
ndiyo njia bora zaidi ya kukabiliana na Ebola, hivyo basi epuka na kuacha uvumi
na usiwe na hofu; inawezekana kupunguza maumivu na kuokoa maisha,” daktari Krishnan
alisema ugonjwa wa virusi vya Ebola (EVD) unazo dalilii zake amabazo ni homa, kuvuja
damu na kuharibika kwa mfumo mkuu wa neva. Maafa ya ugonjwa huu huweza kufikia
hadi asilimia tisini- lakini mzuko wa hivi punde unasababisha maafa ya 55% .
Ugonjwa
huo huchukua muda wa siku ishirini na moja kukomaa. Hakuna kinga wala tiba, bali
huduma za msaada na kudhibiti kupoteza maji mwilini kutokana na kuharisha au kutapika
husaidia katika kuponaInafikiriwa kuwa popo ndo vilemea vya ugonjwa huo.