2014-08-28 15:43:35

Papa atuma rambirambi kwa kifo cha Albert Reynolds


Kufuatia kifo cha Taoiseach Albert Reynolds aliyekuwa Waziri Mkuu wa Ireland, aliye fariki Agosti 21, 2014, Baba Mtakatifu Francisko, alipeleka salaam zake za rambirambi kwa Mke wa Marehemu Reynolds, watoto wake na familia yake. Hati ya rambirambi za Papa, ilitiwa sahihi na Katibu wa Jimbo la Papa, Kardinali Pietro Parolin. Salaam hizo zilizomwa hadharani siku ya Jumatatu wakati wa mazishi ya Marehemu Taoiseach Alibert, baada ya Ibada ya Misa na Maziko iliyoongozwa na Askofu Mkuu Diarmuid Martin, wa Jimbo Kuu la Dublin, katika Kanisa la Moyo Mtakatifu la Donnybrook, Dublin.

Katika rambirambi hizo, Papa alionyesha ukaribu wake kwa familia Reynolds na kutoa baraka zake za kichungaji pia kwa wote waliohudhuria mazishi hayo.

Reynolds, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 81, anakumbukwa kwa kazi kubwa aliyoifanya wakati wa mchakato wa kutafuta amani Ireland ya Kaskazini, na wakati wa utawala wa kihistoria wa kijeshi ya Ireland, na kusitishwa kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994. Alikuwa Waziri Mkuu tangu Februari 1992 hadi Desemba 1994.









All the contents on this site are copyrighted ©.