Mshikamano wa kiekumene katika kuwahudumia wakimbizi na wahamiaji
Baraza la Makanisa Ulimwenguni kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 5 Septemba, 2014 litafanya
semina kwa ajili ya viongozi wa Kanisa, itakayoongozwa na kauli mbiu “Tathmini ya
ya taalimungu ya kiekumene kwa ajili ya viongozi wa Makanisa ya wahamiaji”.
Semina
hii itafanyika kwenye Chuo cha Kiekumene cha Bossey, kilichoko nchini Uswiss. Hii
itakuwa ni nafasi kwa viongozi wa Makanisa kuonesha mshikamano kwa kuwa wamoja. Semina
hii itahudhuriwa pia viongozi wa mashirika ya kiraia.
Washiriki hawa wanatoka
hususan nchini Sierra Leone, Nigeria, Togo na Guyana, lakini ni viongozi wanaowahudumiwa
wakimbizi na wahamiaji wanaoishi Barani Ulaya. Dr. Amèlè Ekuè, mratibu wa semina hii
anasema kwamba, uhamiaji ni kati ya changamoto za kimataifa kwa nyakati hizi, kwani
kuna watu wanalazimika kuzikimbia au kutafuta maisha bora zaidi ughaibuni kutokana
na na vita, athari za mabadiliko ya tabianchi, dhuluma na nyanyaso.
Ni watu
wanaohitaji ulinzi na haki zao kuthaminiwa na Jumuiya ya Kimataifa. Ongezeko la makundi
makubwa ya wahamiaji na wageni, imekuwa ni fursa ya ujenzi wa mshikamano wa kiekumene
anasema Mama Ekuè.
Umefika wakati wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni kuiangalia
changamoto hii, kumbe wakati wa semina kwa viongozi wa wahamiaji mambo kadhaa yatajadiliwa.
Hii ni pamoja na kushirikishana uzoefu na mang’amuzi yao kuhusu hali ya wahamiaji,
changamoto zilizopo, mafanikio na matatizo katika utume wao miongoni mwa wahamiaji
na wakimbizi katika Makanisa yao. Wajumbe wataangalia mikakati inayoweza kuboresha
taalimungu ya kiekumene kuhusu utume wa Makanisa miongoni mwa wa wahamiaji.