2014-08-22 11:59:31

Yapita miaka hamisini ya mauaji ya Mwenye Heri Marie-Clementine Anuarite Nengapeta


Katika tukio la kuadhimisha kutimia miaka 50, tangu Mwenye Heri Marie Clementine Anuarite Negapeta kukabiliwa na kifo dini, Kanisa Katoliki Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, litafanya kilele cha maadhimisho ya jubilee hii katika Makazi Shirika la Familia Takatifu, Kisangani.

Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu, Padre Leonard Santedi, Jumatano wiki hii, aliwasilisha kwa waandishi wa habari, ratiba ya jubilee hii , kwamba, kwanza kutakuwa na mipango mfululizo ya kuongeza uelewa zaidi juu ya maisha ya Sista Nengapeta kwa ajili ya kukuza moyo wa ibada, pili, itakuwa ni hija ya kitaifa katika madhabahu ya Isiro na Wamba na tatu ni kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa Kuu la Isiro, ambalo ilitapewa heshima ya Mashahidi wafia dini.

Padre Santedi, katika taarifa yake kwenye ukurasa wa www.laprosperiteonline.net portal, amesisitiza kwamba, Mwenye Heri Nengapeta, shahidi mfia dini, ni mfano wa maisha maongofu si tu kwa Waktoliki , lakini kwa watu wote wa Kongo. Na pia ni sura ya heshima na uaminifu katika utendaji wa kazi.
Sista Marie-Clémentine Anuarite Nengapeta,alitekwa nyara waasi katika miaka ya 1960, akiwa pamoja na Masista wenzake, na alikataa katakata kutenda dhambi ya kuzini na Kanali Ngalo, hadi kuuawa akiitetea imani yake. Alichagua kifo kuliko kutenda dhambi. Na hivyo, kabla ya kifo chake alikabiliwa na mateso ya makali ya kimwili hadi alipofariki Desemba 1, 1964.
Katika maadhimisho ya miaka 50 ya mauaji Sista Nengapeta, Maaskofu Kongo wanataka kuongeza ufahamu miongoni mwa waamini juu ya fadhila ya mtawa huyo.








All the contents on this site are copyrighted ©.