Wafuasi wa Papa Francisko kwenye mtandao kwa sasa wamevuka millioni 15
Baba Mtakatifu Francisko tangu kuchaguliwa kwake kuliongoza Kanisa Katoliki ameendelea
kutumia mitandao ya kijamii kama njia ya kuwasiliana na watu moja kwa moja. Mtandao
wa twitter ya Baba Mtakatifu, ulifunguliwa na Papa mstaafu Benedikto XVI kunako Desemba
2012. Takwimu zinaonesha kwamba, hadi sasa wafuasi wa Baba Mtakatifu Francisko kwenye
mtandao wake wa twitter wamevuka millioni 15.
Wafuasi wa Baba Mtakatifu katika
lugha ya Kihispania wanaongoza kwa idadi ya watu 6, 479, 550. Wanafuata watumiaji
wa lugha ya Kiingereza ambao idadi yao kwa sasa imefikia wafuasi 4, 366, 300. Wafuasi
wanaotumia lugha ya Kiitalia ni 1, 867, 400. Wafuasi wanaotumia lugha ya Kireno ni
1, 123, 800; watumiaji wa lugha ya Kifaransa ni 291, 800; wanaotumia lugha ya Kilatini
ni 271, 600; Kipolandi ni 251, 100 na Kiarabu wamefikia wafuasi 145, 500.