2014-07-31 12:05:21

Cheche za makubaliano ya amani zaanja kujionesha Msumbiji


Serikali ya Msumbiji na Chama cha upinzani cha RENAMO zimetiliana sahihi mkataba wa amani na hivyo kung'oa mzizi wa fitina ulioibuka kwa kasi kubwa katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita kiasi cha kuzua hofu ya kuzuka tena kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Msumbiji.

Makubaliano haya yamefikiwa baada ya majadiliano ya muda mrefu kati ya Serikali na RENAMO na hivyo kuanza kuweka mikakati ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika nchini humo tarehe 5 Oktoba 2014. Pande hizi mbili zinaendelea kujadiliana namna ya kutekeleza makubaliano ya pande hizi mbili. Chama cha upinzani cha RENAMO kimemteuwa Alfondo Dhlakama kupeperusha bendera ya chama hiki wakati wa kinyang'anyiro cha Urais nchini Msumbiji.







All the contents on this site are copyrighted ©.