2014-04-18 10:27:39

Kardinali Roger Etchegaray kutunukiwa tuzo la Msalaba wa heshima!


Bwana Manuel Valls, Waziri mkuu wa Ufaransa, ni kati ya wageni mashuhuri wanaotarajiwa kuhudhuria katika Ibada ya Misa Takatifu wakati wa kuwatangaza wenyeheri: Yohane wa XXIII na Yohane Paulo II kuwa watakatifu, hapo tarehe 27 Aprili 2014, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Ibada inayotarajiwa kuongozwa na Baba Mtakatifu Francisko.

Akiwa mjini Roma, Waziri mkuu wa Ufaransa anatarajiwa kumtuza Kardinali Roger Etchegaray, Rais mstaafu wa Baraza la Kipapa la Utamaduni Msalaba wa Heshima, kwa kutambua mchango wake katika kukuza na kuendeleza utamaduni ndani na nje ya Kanisa. Hii ni heshima ya hali ya juu kutolewa na Serikali ya Ufaransa kwa watu ambao wamejipambanua kutokana na mchango wao kwa Nchi na Jumuiya ya Kimataifa.







All the contents on this site are copyrighted ©.